1 Samueli 7:15-17 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Samueli alikuwa mwamuzi wa Israeli maisha yake yote.

16. Kila mwaka Samueli alitembelea Betheli, Gilgali na Mizpa, na kuwaamua Waisraeli katika miji hiyo yote.

17. Kisha, alikuwa akirudi Rama, maana huko kulikuwa nyumbani kwake; aliwaamulia Waisraeli haki zao huko, na kumjengea Mwenyezi-Mungu madhabahu huko.

1 Samueli 7