1 Samueli 2:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Halafu Hana aliomba na kusema:“Namshangilia Mwenyezi-Mungu moyoni mwangu.Namtukuza Mwenyezi-Mungu aliye nguvu yangu.Nawacheka adui zangu;maana naufurahia ushindi wangu.

2. “Hakuna aliye mtakatifu kama Mwenyezi-Mungu;hakuna yeyote aliye kama yeye;hakuna aliye mwamba kama Mungu wetu.

3. Acheni kujisifu,acheni kusema ufidhuli.Maana ajuaye ni Mwenyezi-Mungu.Yeye huyapima matendo yote.

1 Samueli 2