23. Maana kwa njia ya neno hai la Mungu, nyinyi mmezaliwa upya, si kama watoto wa baba awezaye kufa, bali baba asiyekufa milele.
24. Kama Maandiko yasemavyo:“Kila binadamu ni kama majani,na utukufu wake wote ni kama ua la majani.Majani hunyauka na maua huanguka.
25. Lakini neno la Bwana hudumu milele.”Neno hilo ni hiyo Habari Njema mliyohubiriwa.