1 Mambo Ya Nyakati 7:19-21 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Wana wa Shemida walikuwa Ahiani, Shekemu, Liki na Aniamu.

20. Hawa ndio wazawa wa Efraimu kutoka kizazi hadi kizazi: Shuthela, Beredi, Tahathi, Eleada, Tahathi,

21. Zabadi na Shuthela. Mbali na Shuthela, Efraimu alikuwa na wana wengine wawili, Ezeri, na Eleadi, ambao waliuawa na wenyeji wa asili wa nchi ya Gathi kwa sababu walikwenda huko kuwanyanganya mifugo yao.

1 Mambo Ya Nyakati 7