1 Mambo Ya Nyakati 6:15-21 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Yehosadaki alikwenda uhamishoni wakati Mwenyezi-Mungu alipowapeleka uhamishoni watu wa Yuda na Yerusalemu kwa kuutumia mkono wa mfalme Nebukadneza.

16. Lawi alikuwa na wana watatu: Gershomu, Kohathi na Merari.

17. Kila mmoja wao pia alikuwa na wana. Gershomu aliwazaa Libni na Shimei;

18. Kohathi aliwazaa Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli;

19. naye Merari aliwazaa Mahli na Mushi. Hizi ndizo jamaa za Walawi kulingana na koo zao.

20. Wafuatao ndio wazawa wa Gershomu kutoka kizazi hadi kizazi: Gershomu alimzaa Libni, Libni akamzaa Yahathi, Yahathi akamzaa Zima,

21. Zima akamzaa Yoa, Yoa akamzaa Ido, Ido akamzaa Zera, Zera akamzaa Yeatherai.

1 Mambo Ya Nyakati 6