1 Mambo Ya Nyakati 25:6-15 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Wanawe wote walipiga muziki kwa matoazi, vinanda na vinubi, kwenye ibada katika nyumba ya Mwenyezi-Mungu wakiwa chini ya uongozi wa baba yao. Asafu, Yeduthuni na Hemani walikuwa chini ya amri ya mfalme.

7. Idadi yao pamoja na wale ndugu zao Walawi waliofundishwa kumwimbia Mwenyezi-Mungu, wote waliokuwa stadi, ilikuwa 288.

8. Wote, wakubwa kwa wadogo, waalimu kwa wanafunzi, walitumia kura katika kupanga kazi zao.

9. Kura ya 1 ilimwangukia Yosefu wa jamaa ya Asafu; ya 2 Gedalia pamoja na ndugu zake na wanawe kumi na wawili;

10. ya 3 Zakuri pamoja na wanawe na ndugu zake kumi na wawili;

11. ya 4 ilimwangukia Seri pamoja na wanawe na ndugu zake kumi na wawili;

12. ya 5 Nethania; pamoja na wanawe na ndugu zake kumi na wawili;

13. ya 6 Bukia; pamoja na wanawe na ndugu zake kumi na wawili;

14. ya 7 Asharela; pamoja na wanawe na ndugu zake kumi na wawili;

15. ya 8 Yeshaya; pamoja na wanawe na ndugu zake kumi na wawili;

1 Mambo Ya Nyakati 25