7. Wana wa Gershoni walikuwa wawili: Ladani na Shimei.
8. Ladani alikuwa na wana watatu: Yehieli mkuu wao, Zethamu na Yoeli.
9. Wana wa Shimei walikuwa watatu: Shelomithi, Hazieli na Harani. Hawa walikuwa viongozi wa ukoo wa Ladani.
10. Wana wa Shimei walikuwa viongozi wanne: Yahathi, Zina, Yeushi na Beria.