1 Mambo Ya Nyakati 23:16-21 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Aliyekuwa mkuu miongoni mwa wana wa Gershomu ni Shebueli.

17. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu; Rehabia, naye alikuwa kiongozi. Lakini Rehabia alikuwa na wana wengi sana.

18. Ishari alimzaa Shelomithi, kiongozi wa kabila zima.

19. Wana wa Hebroni walikuwa wanne: Mkuu wao alikuwa Yeria, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli na wa nne Yekameamu.

20. Wana wa Uzieli walikuwa wawili: Mika mkuu wao, na Ishia wa pili.

21. Merari alikuwa na wana wawili: Mali na Mushi. Wana wa Mali walikuwa wawili: Eleazari na Kishi.

1 Mambo Ya Nyakati 23