16. Aliyekuwa mkuu miongoni mwa wana wa Gershomu ni Shebueli.
17. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu; Rehabia, naye alikuwa kiongozi. Lakini Rehabia alikuwa na wana wengi sana.
18. Ishari alimzaa Shelomithi, kiongozi wa kabila zima.
19. Wana wa Hebroni walikuwa wanne: Mkuu wao alikuwa Yeria, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli na wa nne Yekameamu.
20. Wana wa Uzieli walikuwa wawili: Mika mkuu wao, na Ishia wa pili.
21. Merari alikuwa na wana wawili: Mali na Mushi. Wana wa Mali walikuwa wawili: Eleazari na Kishi.