1 Mambo Ya Nyakati 19:8-11 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Naye Daudi aliposikia habari hizo alimtuma Yoabu na jeshi lote la mashujaa.

9. Waamoni walitoka wakajipanga kwenye lango la mji, hali wale wafalme waliokuja walikuwa peke yao kwenye tambarare.

10. Yoabu alipoona kuwa vita ni vikali dhidi yake, mbele na nyuma, aliwateua baadhi ya wanajeshi hodari zaidi wa Waisraeli, akawapanga kukabiliana na Waaramu.

11. Wale wanajeshi wengine waliobaki, aliwaweka chini ya uongozi wa Abishai ndugu yake, naye akawapanga ili wakabiliane na Waamoni.

1 Mambo Ya Nyakati 19