1 Mambo Ya Nyakati 16:20-36 Biblia Habari Njema (BHN)

20. mkitangatanga toka taifa hadi taifa,kutoka nchi moja hadi nchi nyingine,

21. Mungu hakumruhusu mtu yeyote awadhulumu;kwa ajili yao aliwaonya wafalme:

22. “Msiwaguse wateule wangu;msiwadhuru manabii wangu!”

23. Mwimbieni Mwenyezi-Mungu, ulimwengu wote.Tangazeni kila siku matendo yake ya wokovu.

24. Yatangazieni mataifa utukufu wake,waambieni watu wote matendo yake ya ajabu.

25. Maana Mwenyezi-Mungu ni mkuu, anasifika sanaanastahili kuheshimiwa kuliko miungu yote.

26. Miungu yote ya mataifa mengine si kitu;lakini Mwenyezi-Mungu aliziumba mbingu.

27. Utukufu na fahari vyamzunguka,nguvu na furaha vyajaza hekalu lake.

28. Mpeni Mwenyezi-Mungu, heshima enyi jamii zote za watu,naam, kirini utukufu na nguvu yake.

29. Mpeni Mwenyezi-Mungu heshima ya utukufu wa jina lake;leteni tambiko na kuingia nyumbani mwake.Mwabuduni Mwenyezi-Mungu patakatifuni pake.

30. Ee dunia yote; tetemeka mbele yake!Ameuweka ulimwengu imara, hautatikisika.

31. Furahini enyi mbingu na dunia!Yaambieni mataifa, “Mwenyezi-Mungu anatawala!”

32. Bahari na ivume, pamoja na vyote vilivyomo!Furahini enyi mashamba na vyote vilivyomo!

33. Ndipo miti yote msituni itaimba kwa furahambele ya Mwenyezi-Mungu anayekujanaam, anayekuja kuihukumu dunia.

34. Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema,kwa maana fadhili zake zadumu milele!

35. Mwambieni Mwenyezi-Mungu:Utuokoe, ee Mungu wa wokovu wetu,utukusanye pamoja na kutuokoa kutoka kwa mataifa,tupate kulisifu jina lako takatifu,kuona fahari juu ya sifa zako.

36. Asifiwe Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli,tangu milele na hata milele!Kisha watu wote wakasema, “Amina!” Pia wakamsifu Mwenyezi-Mungu.

1 Mambo Ya Nyakati 16