4. Yafuatayo ndio majina ya watoto aliozaa huko Yerusalemu: Shamua, Shobabu, Nathani, Solomoni,
5. Ibhari, Elishua, Elpeleti,
6. Noga, Nefegi, Yafia,
7. Elishama, Beeliada na Elifeleti.
8. Wafilisti waliposikia kwamba Daudi amepakwa mafuta kuwa mfalme wa nchi nzima ya Israeli, wote walitoka kwa wingi kwenda kumtafuta. Daudi alipopata habari, alitoka kwenda kuwakabili.
9. Wafilisti walifika wakaanza mashambulizi katika bonde la Refaimu.